Plan Info
Soma Biblia Kila Siku 03/2024Sample
Mungu hutumia wajumbe akitengeneza nyumba yake hapa duniani, yaani watu wake. Katika agano la kale mjumbe alikuwa ni Musa, katika agano jipya ni Yesu. Wote wawili walithibitika kuwa waaminifu katika kazi yao. Lakini Yesu ana heshima zaidi ya Musa, kama kazi yake ilivyo na maana zaidi. Wakati Musa alikuwa ni mtumishi tu, Yesu ni Mwana wa Mungu. Kwa hiyo tumzingatie sana Yesu. Yeye ndiye fahari na tumaini la nyumba takatifu ya Mungu ambamo sisi tumo kama tukishikamana naye kwa imani mpaka mwisho.
Scripture
About this Plan
Soma Biblia Kila Siku 03/ 2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Machi pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha ...
More